Habari

Tosci yatakiwa kuweka mkazo ukaguzi mbegu,mashamba

“Rai yangu kwenu ni kuimarisha ukaguzi ili mkulima  anufaike na mbegu bora.”

Amesema serikali itahakikisha inaendelea kuwekeza katika vifaa na miundombinu bora ili kurahisisha jukumu hilo sambamba na kuwajengea uwezo watumishi wa TOSCI ili waweze kutekeleza majukumu yao kiufanisi kwa kufuata misingi ya utaalamu wa kazi yao.

 Serikali kupitia Wizara ya Kilimo itaendelea kutafuta fursa mbalimbali nje ya nchi na kuwawezesha Wataalam wengi zaidi wa TOSCI kwenda kujifunza ili kuleta manufaa zaidi kwa tasnia ya mbegu na Taifa kwa ujumla.

Ninawapongeza sana kwa kazi kubwa ya maboresho ya maabara na ujenzi wa maktaba,ni imani yangu k ofwamba hatua hii itaongeza zaidi ufanisi katika kutekeleza majukumu yenu”Alisema Mavunde

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya TOSCI, Patrick Ngwediagi alibainisha mafanikio ya Taasisi yake ikiwemo kuongezeka kwa mbegu zilizothibitishwa ubora, kupungua kwa mbegu feki kunakotokana na matumizi ya lebo za kielektroniki na kuongeza uzalishaji wa ndani wa mbegu kulinganisha na zinazoagizwa

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button